Thursday, July 6, 2017

Wananchi wenye bima za Afya kuzikwepa hospital za Serikali

kadi ya Bima ya Taifa ya Afya (NHIF)Kukosekana kwa kauli za kiungwana na huduma kwa wagonjwa kwenye baadhi ya hospitali za serikali kumetajwa kuwa ni mambo yanachosababisha wagonjwa wengi wanaopata huduma kwa kupitia Bima ya Afya kuzikimbia hospitali hizo na kwenda kwenye hospitali binafsi na mashiriki ya kidini.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko Taifa wa Bima ya afya, Spika Mstaafu Anna Makinda, ameeleza hayo katika hafla ya uzinduzi wa huduma za karibu unatolewa na Madaktari Bingwa kutoka hospitali za Kanda hapa nchini ukiwa ni mkakati unaoratibiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Tatizo la wananchi wengi kutoelewa umuhimu wa huduma ya Bima ya Afya kiasi cha kutojiunga nao ,nalo linaonekana kuutia dosari mkoa wa Rukwa, Mkuu wa mkoa huo Zelote Stephen Zelote ametoa wito kwa wananchi wake kujiunga na huduma za bima ya afya, Mwakilishi wa Mkurugenzi NHIF katika hafla hiyo ameelezea umuhimu wa huduma za madaktari bingwa kufanywa katika mikoa ya pembezoni kama vile Rukwa, wanufaika wakitoa shukrani kwa mfuko wa Bima.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...