Thursday, July 6, 2017

Matangazo kwenye miito ya simu, TCRA yapiga marufuku, ni ukiukwaji wa sheria

TCRAMamlaka ya mawasiliano Tanzania – TCRA imewataka watoa huduma za mawasiliano wote kusitisha mara moja utoaji wa matangazo kwenye huduma za mawasiliano yasiyozingatia kanuni za huduma za ziada za mwaka 2015 kuanzia leo juni 6 ikiwemo huduma za matangazo yanayotolewa na watoa huduma wakati wa kupiga simu hususani kabla ya simu kuita.
Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba baada ya TCRA kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wadau mbalimbali wa mawasiliano wakionesha hisia zao kwa kukerwa na matangazo yanayotokea wakati wa miito ya simu kabla ya kuunganishwa mpigaji na mpokeaji, ama wakati mpokeaji anapoongea na simu nyingine au mpokeaji akiwa hapatikani kwa wakati huo, kitendo ambacho ni cha kupoteza muda lakini pia kumpa mtumiaji wa simu matangazo hayo bila idhini yake.
Sambamba na agizo hilo, watoa huduma pia wameonywwa kwa kutoa matangazo kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno bila ya ridhaa ya wateja wao kitendo ambacho ni kinyume cha matakwa ya kanuni za huduma za ziada mwaka 2015 na kanuni za kumlinda mtumiaji za mwaka 2011.
Aidha Mhandisi Kilaba amefafanua jinsi ambavyo kanuni za huduma za ziada zinawataka watoa huduma wazingatie.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...