Thursday, July 6, 2017

Wananchi wadai fidia bomba la mafuta

56d6cf8ba4a55Wananchi wa kata ya Chongoleani ambao maeneo yao yataathiriwa na mradi wa bomba la mafuta wameiomba serikali kuharakisha mchakato wa kulipa fidia ili waweze kujianda na kuanzisha shughuli mbadala zitakazo waingizia kipato.
Ombi hilo wamelitoa kwa mkuu wa mkoa wa tanga Martin Shigela katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.
Wamesema ulipaji wa fidia ukifanyika mapema utawasaidia wananchi kuanza maandalizi ya kuanzisha miradi ambayo itaendana na mahitaji ujio wa mradi wa bomba la mafuta kutoka nchini Uganda hadi bandari ya Tanga.
Akizungumza katika mkutano huo mkuu wa mkoa amewapongeza wananchi kwa uvumilivu wao na kuwatoa hofu kuhusu ulipwaji wa fidia na kwamba wakati ukifika kila mmiliki wa eneo atalipwa haki yake kulingana tathimini iliyofanywa.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...