Saturday, July 8, 2017

Nyara za serikali zenye thamani ya shilingi milioni 33 kukamatwa

C6NLR1OWUAAljJn
Jeshi la polisi mkoani Morogoro linawashikilia watu wawili kwa makosa mawili tofauti yakiwemo ya kukutwa na dawa za kulevya na pembe za ndovu zenye thamani zaidi ya shilingi million 33.
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro Ulrich Matei amesema askari wakiwa katika doria walipokea taarifa kutoka kwa raia wema walifanikiwa kumkamata Kibosa Kibona mkazi wa Mlali wilayani Mvomero ambapo amekutwa na pembe za ndovu mbili zenye thamani zaidi ya shilling million 33.
katika tukio lingine kamanda matei amesema jeshi la polisi limefanikiwa kumukamata Sande Balinusi maeneo ya Msamvu manispaa ya morogoro baada ya kumpekua na kukutwa na kiloma moja ya dawa za kulevya aidha watuhumiwa wao watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...