Saturday, July 8, 2017

Jamii nchini imeshauriwa kuwafariji wafungwa kwa kuwatembelea na kuwapa misaada

wafungwa-25-wauawa-brazil-640x330Jamii nchini imeshauriwa kuwafariji wafungwa kwa kuwatembelea na kuwapa misaada ya kibinadamu ili waweze kukidhi mahitaji yao kutokana na ukweli kwamba serikali peke yake haina uwezo wa kumkamilishia kila mfungwa mahitaji yake awapo gerezani.
Wito huo umetolewa na mkuu wa gereza la mahabusu Sumbawanga mara baada ya kupokea msaada wa mahitaji ya kibinadamu kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa akiongoza kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Kalambo akikabidhi msaada huo, amewapongeza askari wa jeshi la magereza kwa kazi ngumu wanayoifanywa kuhakikisha wafungwa wako salama wakati wote na kueleza nia ya kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kalambo kufika gerezani hapo.
Vitu vilivyokabidhiwa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kalambo kwa mkuu wa gereza la mahabusu Sumbawanga, baadhi yake ni sabuni, miswaki, dawa ya meno, mafuta ya kupakaa, nyembe na kalamu za kuandikia maaskari wawapo kazini.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...