Ni marufuku inayotekeleza agizo la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli la kutaka shughuli zote za uchimbaji wa madini pamoja na utafiti wake kuwa chini ya kamati za ulinzi na usalama ya maeneo husika ambapo mkuu wa wilaya ya hanang anatoa maagizo haya kwa kampuni ya Kudu Resource Kampani ya utafiti wa madini ya dhahabu katika eneo la Basotulengo likiwa ni kuepusha migogoro mbalimbali baina ya wananchi na wawekezaji katika maeneo ya machimbo.
Nao uongozi wa basotu wakatoa ushauri huu kwa serikali wakilenga zaidi kwa rais.
Hivi karibuni inaelezwa wananchi wamevamia eneo hili kwa kuitaka kampuni hii kutekeleza baadhi ya ahadi zake kwa wananchi wa eneo la basotu ambazo waliziahidi kabla ya kuanza kwa utafiti ambapo ni pamoja na barabara,na kuchimba visima vya maji kwaajili ya wakaazi wa basotu.
No comments:
Post a Comment