
Idara inayohusika na safari za ndege
nchini Marekania FAA ,inachungunza kisa ambapo ndege ya shirika la Air
Canada nusura igonge ndege zingine katika uwanja wa San Franciso.
Shirika
hilo linasema kuwa ndege ya AC759 ikitokea Toronto iliruhusiwa kutua
siku ya Ijumaa lakini rubani akajianda kutua katika barabara ambapo
ndege zingine zilikuwa zinajianda kupaa.Waelekezi wa safari za ndege waliweza kufahamu tatizo hilo na kumuamrisha rubani kupaa tena ili kujiandaa kutua kwa kwa mara ya pili.Kisha ndege hiyo ikaweza kutua salama.
FAA kwa sasa inachunguza umbali uliokuw kati ya ndege ya Air Canada na ndege iliyokuwa ikijiandaa kupaa.
Kisa hicho kinatajwa kuwa kisicho cha kawadia.
Air Canada inasema kuwa abiria 135 na wahudumu 5 walikuwa ndani ya ndege hiyo.
Haijulikani ni watu wangapi waliokuwa ndani ya ndege nne zilizokuwa kwenye barabara ya kupaa.
![]() |
| Nusura ndege ya Canada igonge ndege nne uwanjani San Francisco |

No comments:
Post a Comment