Wednesday, July 12, 2017

Makamu Rais Yemi Osinbajo amtembelea Buhari London

Muhammadu Buhari na makamu Rais Yemi Osinbajo Abuja Machi 13,2017Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari ambae yuko London kwa ajili ya matibabu, amefanya mkutano wake wa kwanza na anaye kaimu nafasi hiyo kwa miezi miwili sasa.

Msemaji wa kaimu Rais, Yemi Osinbajo, ameelezea kuwa mkutano huo ulikuwa mzuri.
Hata hivyo, hakutoa maelezo zaidi.
Buhari alirejea kazini mwezi Machi baada ya matibabu London
Buhari amekuwa jijini London tangu mwezi Mei, akipata matibabu kwa ugonjwa ambao haujatajwa.
Bwana Osinbajo anategemewa kurudi nchini Nigeria baada ya mkutano huo.
 Ukimya wake umeibua mjadala nchini Nigeria iwapo Buhari ataweza kurudi na kuendelea na majukumu yake ama la.
Buhari akiwa na familia yake mwezi Machi
Buhari akiwa na familia yake mwezi Machi

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...