Hakuna namna yoyote ya kuacha kufika katika mto Ruvuma ambao una mamba wanaokamata watu,kukosekana kwa maji ya bomba vijijini mwao vinawafanya wakazi wa vijiji jirani kutumia maji ya mto huo kwa matumizi yote ya binadamu. Tayari watu kumi na tisa wameripotiwa kuuawa na mbamba katika mto huo huku wengine wakipata majeraha na ulemavu wa kudumu.
Hamisi Mpunga ni mtoto na mkazi wa kijiji cha Sindano aliyejeruhiwa na mamba kwenye mkono wake wa kuume tangu mwaka 2013 akiwa anavua samaki anaugulia maumivu hadi sasa,huku wazazi wake wakikosa uwezo wa kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi.
Serikali inaombwa kuwasaidia wakazi hao ili wasiendelee kuzulika na mamba katika mto wanaoutegemea kwa maji ya kunywa na shughuli za kilimo.
No comments:
Post a Comment