Monday, July 10, 2017

Kaya Elfu 10 kukosa makazi Tabora, Nyumba kubomolewa, zipo kwenye hifadhi ya reli

Image result for bomoa bomoa taboraZaidi ya kaya elfu kumi ziko hatarini kukosa makazi kutokana na nyumba zao za kuishi kujengwa katika eneo la shirika la reli TRL baada ya kuwekewa alama ya kuvunjwa ili kupisha ujenzi wa reli ya kisasa na miundo mbinu mingine . Baadhi ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya mkoa wa Tabora ambao nyumba zao zimewekewa alama ya kuvunjwa wakiwa katika nyuso za huzuni wameeleza masikitiko yao huku baadhi yao wakidai kuwa hawana mahali pa kwenda.
Mbali na kueleza masikitiko yao zaidi wanaelekeza kilio hiki kwa serikali wakihitaji msaada.
Wananchi hawa wamepewa notis na shirika la reli Tanzania kuhakikisha wanavunja nyumba hizo ndani ya siku thelathini kabla ya kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria.
Sakata hili la bomoa bomoa limeathiri maeneo mengi ya mkoa wa Tabora lakini kata zilizoathirika zaidi ni CHEYO, ISEVYA, KILOLENI , BACHU na MAPAMBANO zote zikiwa katika manispaa ya Tabora.
Image result for bomoa bomoa taboraRelated imageImage result for bomoa bomoa taboraRelated image

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...