Friday, July 7, 2017

Watu 8 wauwawa kwenye mkanyagano uwanja wa mpira Malawi

Watu 8 wauwawa kwenye mkanyagano uwanja wa mpira Malawi
Watu 8 wauwawa kwenye mkanyagano uwanja wa mpira Malawi
Watu wanane wakiwema watoto saba wameuwawa kwenye mkanyagano kabla ya kufanyika kwa mechi ya kandanda nchini Malawi.
Watu wengine zaidi walijeruhiwa wakati wa mkanyagano huo ulitokea uwaja wa Bingu mjini Lilongwe.
Mkanyagano huo unaripotiwa kutokea wakati maefu ya watu walijaribu kutafuta viti kabla ya mchuano wa kirafiki kati vilabu vikubwa vya Nyasa Big Bulets na Silver Strikers.
Mwandishi wa BBC aliye Malawi anasema kwa milango ya uwanja huo unaowachukua watu 40,000 ilistahili kufunguliwa kuruhusu watu kuingia mapema lakini ilichelewa kwa muda wa saa tatu.
Hata hivyo maelfu walikwa wamefika na baadhi walijaribu kuingia kwa nguvu hali iliyosababisha polisi kufyatua vitoa machozi.
Inspekta wa polisi aliliambia shirika la Reuters kuwa anatarajia idadi wa waliokufa kuongezeka.
Rais Peter Mutharika ametuma rambi rambi zake na kusema kuwa serikali inafanya kila iwezalo kuzisadia familia za waliouawa.
map
Watu 8 wauwawa kwenye mkanyagano uwanja wa mpira Malawi

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...