Friday, July 7, 2017

Trump aitaka Urusi kuwacha kuivuruga Ukrain

Donald Trump (left) with Andrzej Duda in Warsaw, 6 July
Trump (kushoto) na rais wa Poland Andrzej Duda
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito kwa Urusi kuacha kuivuruga Ukrain na nchi zingine, na kuacha kuungia mkono tawala dhalimu kami zile za Styria na Iran.
Akiongea akiwa mji mkuu wa Poland Warsaw, Trump aliitaka Urusi kujiunga na mataifa yenye kuwajibika.
Urusi imepinga matamshi hayo ya Trump.
Mr and Mrs Trump arrive in Hamburg
Bwana Trump akiwasili Hamburg kwa mkutano wa G20
Rais huyo wa Marekani amesafiri kuenda mjini Hamburg kuhudhuria mkutano wa G20 ambapo atakutana na rais wa Urusi kwa mara ya kwanza.
Mjini Warsaw alihutubia umati mkubwa uliokuwa ukimshangilia
Aliisifu Poland kama nchi iliyo tayari kulinda uhuru wa magharibi.
People holding portraits of US President Donald Trump and Polish President Andrzej Duda wait at Krasinski Square in Warsaw, 6 July
Watu wanaosikiliza hotuba ya trump Poland
Bwana Trump aliitaka Urusi kuungana na nchi zinaowajibika katika vita dhidi ya adui mmoja.
Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov alisema kuwa Urusi haijakubali kuwa inavuruga eneo hilo.
Anti-capitalism activists wearing masks of UK Prime Minister Theresa May (L) and US President Donald Trump protest in Hamburg, 6 July
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May na rais wa Marekani Donald Trump wakikejeliwa Hamburg on Thursday
Trump ametofautiana na baadhi ya nchi za ulaya kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa na biashara,
Mashirika ya kutoa misaada yatarajiwa kufanya maandamano mjini Hamburg kuwakata viongozi kujitahidi zaidi kumaliza kutokuwepo usawa.
Activists arrive at Hamburg central railway station, 6 July
Waandamani wawasili kwa traini mjini Hamburg
Polish First Lady Agata Kornauser-Duda (R) and US First Lady Melania Trump (L) during a tete-a-tete meeting in Belweder Palace in Warsaw, 6 July
Melania Trump (kushoto) akiwa na mama wa taifa nchini Poland Agata Kornauser-Duda

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...