
Waziri wa mawasiliano nchini Somalia
ametangaza kuwa tatizo la kupotea kwa intaneti, kwa muda wa karibu wiki
mbili sasa ni janga kubwa kwa uchumi wa nchi hiyo.
Abdi Anshur
Hassan, aliiambia radio ya taifa kuwa nchi inapoteza takriban dola
milioni 10 kwa siku kutokana na kukatika kwa internet na hadi sasa nchi
imepoteza dola milioni 130.Tatizo hilo lilisababishwa na kuharibiwa kwa nyaya za chini ya bahari zaidi ya wiki mbili zilizopita, kwa mujibu wa Radio Mogadishu.
Hata hivyo Bwana Hassan anasema kuwa serikali inafanya kila iwezalo kurejesha huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment