![]() |
| Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi akiwapongeza baadhi ya makamanda waliofanikisha ushindi huo |
Mosul ndipo kundi la wapiganaji wa kiislamu IS lilipotangaza kuunda uongozi wake miaka mitatu iliyopita
![]() |
| Mwanamke huyu na familia yake ni miongoni mwa waliopoteza makazi yao kutokana na vita |
Bwana Abadi amekuwa akitembea katika barabara za mji wa Mosul na kuwapongeza wanajeshi.
![]() |
| Muonekano wa mji wa Mosul baada ya vita |
Mwanzoni kulikuwa na taarifa za kuwepo mapigano, na moshi mzito ukionekana juu ya eneo ambao limekuwa ndio kitovu cha wapiganaji wa IS.
Kundi hilo bado linahodhi sehemu ya magharibi na Kusini mwa Mosul na inaaminika litaendelea kufanya mashambulizi katika sehemu kubwa ya Iraq
![]() |
| Wanajeshi wa Iraq walipambana usiku kucha kuukomboa mji huo |
Maelfu ya raia wamekimbia huku wengine wakikosa pa kukimbilia wakati mapigano yakiendelea.




No comments:
Post a Comment