Tuesday, July 11, 2017

Haider al-Abadi: Mosul bado ina changamoto nyingi

Haider al-Abadi alitembelea mji huo baada ya mapigano kumalizikaWaziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi, ametahadharisha kwamba kuna changamoto nyingi, licha ya ushindi katika mapambano ya kuurudisha mji wa Mosul kutoka katika himaya ya wapiganaji wa Kiislamu.
Mapigano ya miezi tisa yameharibu mji wa Mosul huku maelfu wakiwa wameukimbia mji huo na wengine wakiachwa bila makazi.
Akizungumza mjini humo, bwana Abadi amesema hivi sasa ni muhimu kurudisha hali ya utulivu.
Mapigano hayo yameuachia mji wa Mosul makovu makubwaKiongozi wa vikosi vinavyoongozwa na Marekani, jenerali Stephen Townsend, amesema vita dhidi ya wapiganaji wa kiislamu bado havijaisha.
Ameitaka serikali ya Iraq kuzungumza na waislamu wa dhehebu la Sunni ili kuepusha kuibuka tena kwa wapiganaji wa IS.

No comments:

Post a Comment

most viwed news

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewata...