
Mwanamuziki wa nyimbo za reggae
nchini Uganda Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine,
anaapishwa leo kama mnunge wa eneo la Kyadondo East
Wine aliwania
kiti hicho kama mgombea huru na kuwashinda wagombea wanne ambapo
alipata kura 25,659 kati ya kura 33,310 zilizopigwa kwenye uchaguzi
mdogo uliofanyika tarehe 29 mwezi Juni.Alisema kuwa anaingia bungeni kama kiongozi na wala si mwanasiasa, kwa mujibu wa gazeti la New Vision.
Chama tawala NRM na upinzani wamekuwa wakimtaka Wine ajiunga na mmoja wao.
Picha ya Wine akimsalamia Rais Museveni wakati wa misa ya mfanyabiashara mmoja ilikosolewa na baadhi ya wafuasi wake katika mitandao.
No comments:
Post a Comment